Arifa ya Ulaghai

Jihadhari na ulaghai unaoashiria kuwa na uhusiano na Umoja wa Mataifa

Umoja wa Mataifa umefahamishwa kuhusu mawasiliano mbalimbali, yanayosambazwa kupitia barua pepe, tovuti za Intaneti, SMS na kupitia barua au faksi za kawaida, yakisema kwa uwongo kwamba yametolewa na, au kwa kushirikiana na Umoja wa Mataifa na/au maafisa wake. Ulaghai huu, ambao unanuia kupata pesa na/au mara nyingi maelezo binafsi kutoka kwa wapokeaji wa mawasiliano kama hayo, ni ya udanganyifu.

Umoja wa Mataifa ungependa kuonya umma kwa ujumla kuhusu shughuli hizi za ulaghai zinazofanywa kwa jina la Shirika hili, na/au maafisa wake, kupitia mipango tofauti ya ulaghai.

  • Umoja wa Mataifa hautozi ada katika hatua yoyote ya mchakato wake wa kuajiri  (kutuma maombi, mahojiano, ushughulikiaji, mafunzo) au ada nyingine, au kuomba taarifa kuhusu akaunti za benki za waombaji.Ili kuomba kazi nenda kwenye careers.un.org and na ubofye Vacancies (Nafasi za Kazi). Angalia maelezo zaidi kuhusu ulaghai unaohusiana na ajira..
  • Umoja wa Mataifa hautozi ada katika hatua yoyote ya mchakato wake wa ununuzi (usajili wa msambazaji, uwasilishaji wa zabuni) au ada nyingine.  Tembelea Kitengo cha Ununuzi na Ugavi ili kuona fursa za hivi punde za biashara na Umoja wa Mataifa.
  • Umoja wa Mataifa hauombi taarifa zozote zinazohusiana na akaunti za benki au taarifa nyingine binafsi.
  • Umoja wa Mataifa hautoi zawadi, tuzo, fedha, vyeti, kadi za mashine ya kutoa pesa kiotomatiki (kadi za ATM), fidia ya ulaghai wa Intaneti, au ufadhili wa masomo, au kuendesha michezo ya bahati nasibu.
  • Umoja wa Mataifa hauidhinishi likizo au pensheni za kijeshi, au kutoa vifurushi badala ya ada. 

Umoja wa Mataifa unapendekeza sana kwamba wanaopokea maombi, kama vile waliofafanuliwa hapo juu wawe waangalifu sana kuhusiana na maombi hayo. Upotevu wa fedha na wizi wa utambulisho unaweza kutokana na uhamishaji wa pesa au taarifa binafsi kwa wale wanaotoa mawasiliano kama hayo ya ulaghai. Waathiriwa wa ulaghai kama huo wanaweza pia kuwaripoti kwa mamlaka za kutekeleza sheria za eneo lao ili wachukuliwe hatua zinazofaa.

Si hati rasmi. Kwa ajili ya maelezo tu.